TANGAZO LA MKUTANO WA HADHARA WA CHAMA CHA MAPINDUZI UTAKAOFANYIKA KATIKA VIWANJA VYA JANGWANI, SIKU YA JUMAMOSI, TAREHE 09-06-2012.
TANGAZO:
Chama Cha Mapinduzi (CCM), Kimeandaa
Mkutano Mkubwa wa Hadhara kwa wananchi wote, Siku ya Jumamosi, tarehe
09/06/2012, Katika Viwanja vya Jangwani Kuanzia saa 8 mchana.
Maudhui; “ Kutoa Msimamo Wake Juu
ya Masuala Yanayogusa Mustakabali wa Taifa. Hivyo Chama Kitatumia Fursa hiyo
Kuelezea Watanzania Juu ya Msimamo Wake Katika Mambo yafuatayo:
1.
Hatma ya maisha ya Watanzania
·
Ajira
·
Miundo mbinu ya Barabara, Reli,
Bandari Na Anga.
·
Bei za bidhaa
mbalimbali.
·
Umeme
·
Rasilimali za taifa
2.
Msimamo wa Chama Cha Mapinduzi kuhusu
Mchakato wa Katiba Mpya.
3.
Vurugu za Zanzibar.
Katika Mkutano huo, Viongozi
mbalimbali wa Chama na Serikali watakuwepo na kutoa ufafanuzi juu ya masuala
hayo yaliyoainishwa kama msimamo wa Chama Cha Mapinduzi.
Chama Cha Mapinduzi, kinawaalika
wanachama wake wote, wakereketwa na wananchi kwa ujumla kuhudhuria katika
mkutano huo mkubwa. Mkutano utafanyika kwa amani na utulivu na wote
mnakaribishwa.
KIDUMU CHAMA CHA
MAPINDUZI
Imetolewa na:
JUMA SIMBA
KATIBU WA SIASA NA
UENEZI
MKOA WA DAR ES
SALAAM.
07/06/2012
JAMAA WAKUTANA NA ADHA YA WANAJESHI ALMAARUFU KAMA WAJEDA.
Kila siku mnaambiwa msipite maeneo yao hawa jamaa lakini raia hamkomi.
wanajeshi
walivyo msuba.............inaweza ndio ikawa shughuli ya siku
nzima.........mkacheza kiduku hapooo hadi maji
yatakapokauka............h awana tatizo na mtu, watapeana zamu ya kwenda kula ila raia ndio mtakausha huo Mto.
KCB TANZANIA YAZINDUA HUDUMA MPYA YA DISPORA BANKING
Mwenyekiti Mtendaji wa Benki ya KCB Tanzania DK Edmund
Mndolwa akizungumza wakati wa hafla ya uzinduzi wa huduma ya KCB DIASPORA
BANKING uliofanyika leo Jijini Dar es Salaam.
Mwenyekiti Mtendaji wa Benki ya KCB Tanzania Dk Edmund
Mndolwa, akizindua rasmi huduma mpya inayotolewa na KCB DIASPORA BANKING,
Katikati ni Mmoja wa Mameneja wa benki hiyo SHOSE KOMBE. Anayeshuhudia ni
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki hiyo MOEZ MIR.
Baadhi ya Wafanyakazi wa Benki
ya KCB Tanzania wakifuatilia kwa makini uzinduzi wa huduma mpya ya KCB DIASPORA
BANKING iliyoanzishwa na benki hiyo wakati wa hafla ya uzinduzi iliyofanyika leo
Jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi wa Masoko na
Mahusiano wa Benki ya KCB Tanzania Christine Manyenye akifafanua kuhusiana na
huduma mpya iliyoanzishwa na benki hiyo ya KCB DIASPORA BANKING wakati wa hafla
ya uzinduzi iliyofanyika leo Jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya Wafanyakazi wa Benki
ya KCB Tanzania wakifuatilia kwa makini uzinduzi wa huduma mpya ya KCB DIASPORA
BANKING iliyoanzishwa na benki hiyo wakati wa hafla ya uzinduzi uliofanyika leo
Jijini Dar es Salaam
Sakata la Mafuta Jijini Mbeya: Mafuta ya Taa Jijini Mbeya ya panda bei kutoka Tsh 2175 mpaka kufikia Tsh 3000 na 3500. Ni Kutokana na uhaba wa Mafuta hayo.
Wananchi
wa Jiji la Mbeya wakiwa wana haha kupata Mafuta ya taa katika kituo cha
mafuta
Baadhi
ya Njinga zikiwa zimepaki eneo ambalo ndilo pekee Mafuta yanapatikana jinini
Mbeya
Mdau
akiwa anatazama vema kama anazo pesa za kununua Mafuta hayo baada ya kushtuka
kuambiwa kuwa bei imepanda mpaka kufikia 3500
Kila
mtu anataka kupata mafuta kwa muda katika eneo hilo Mpaka wenye mapipa nao
wamo.
KAMATI ZA BUNGE ZAENDELEA NA KAZI YA KUPOKEA MAKADIRIO YA BAJETI ZA WIZARA LEO
Waziri
wa Elimu na Mafunzo ya Ufunzo Mhe. Shukuru Kawambwa akiwasilisha makadirio ya
bajeti ya Wizara yake mbele ya Kamati ya Huduma za Jamii kabla ya kupelekwa
Bungeni. Kulia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Huduma za Jamii Mhe. Magareth Sitta na
Makamu Mwenyekiti wa Kamati hiyo Dkt. Faustine Ndugulile.
Makamu
Mwenyekiti wa kamati ya Huduma za Jamii Mhe. Faustine Ndugulile (kushoto) na
Mwenyekiti wa kamati hiyo Mhe. Magareth Sitta (katikati) wakimsikiliza kwa
makini Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufunzo Mhe. Shukuru Kawambwa alipokuwa
akiwasilisha makadirio ya bajeti ya Wizara yake mbele ya kamati hiyo
leo.
Mwenyekiti
wa Kamati ya Bunge ya Maendeleo ya Jamii Mhe. Jenister Mhagama akisisitiza jambo
wakati wakipokea makadirio ya bajeti ya wizara ya kazi na Ajira iliyo wasilishwa
mbele ya kamati hiyo. Kushoto kwake ni Makamu Mwenyekiti wa Kamati hiyo Mhe.
Juma Nkamia na Kulia ni Katibu wa Kamati hiyo Chacha Nyakega, Waziri wa Kazi na
Ajira Mhe. Gaudensia Kabaka na naibu waziri wa Wizara ya kazi na Ajira Mhe. Dkt
Milton Makongoro Mahanga.
Mwenyekiti
wa Kamati ya fedha na Uchumi Mhe. Andrew Chenge akifafanua jambo mbele ya
wajumbe wakamati na watendaji kutoka wizara ya fedha baada ya kupokea
mapendekezo ya bajeti ya wizara ya fedha yaliyo wasilishwa mbele ya kamati hiyo
leo. Kulia kwake ni Waziri wa fedha Mhe. William Mgimwa Mhe Saada Mkuya Salum na
Mhe Janet Mbene, amabo ni Manaibu waziri katika wizara hiyo.
Mjumbe
wa kamati ya Hesabu za Mashirika ya Umma Mhe.Murtaza Ally Mangungu akifurahia
jambo baada ya kupokea hesabu zilizokaguliwa za chuo cha Elimu ya Biashara (CBE)
kwa mwaka 2010/2011. Kulia kwake ni Mwenyekiti wa Kamati hiyo Mhe. zitto Kabwe
na Kushoto ni Katibu wa Kamati hiyo Erick Maseke
kamati
ya POAC ikiendelea na kazi.
Picha zote na Owen Mwandumbya wa Bunge
Picha zote na Owen Mwandumbya wa Bunge
AUWA NA KISHA KUNYOFOLEWA UUME, NA MIKONO MKOANI ARUSHA
KAMANDA WA POLISI WA MKOA WA ARUSHA LIBERATUS SABAS
(NA GLADNESS MUSHI WA FULLSHANGWE-ARUSHA)
Mtu mmoja ambaye hajajulikanan jina lake
amefarikidunia huku baadhi ya viungo vyake hasa sehemu za uume wake
zikiwa zimechomolewa pamoja na mikono yake
Akiongea na waandishi wa habari mapema leo kamanda wa polisi mkoa wa arusha Sabas Liberatus alisema kuwa tukio hilo lilitokea may 26 majira ya saa tni asubuhi katika eneo la Mto Nambala wilyani Arumeru
Kamanda Sabas alisema kuwa katika siku ya tukio mytu mmoja mwenye
jinsia ya kiume ambaye hajatambulika mpaka sasa anakadiriwa kuwa na
miaka25-30 alikutwa akiwa amefariki
Kamanda huyo aliongeza kuwa mara baada ya wapita njia kumkuta
akiwa amefariki waligundua kuwa pia hana viungo mbalimbali ndani ya
mwili wake hali ambayo ilizua tafrani kubwa
‘hawa watu walipomuangalia kwa undani sana waliweza kujua na
kutambua kuwa baadhi ya viungo vyake havipo na ndipo walipota taarifa
kwa jeshi la polisi na sisi tulipoofika ndani ya eneo la tukio
tuliyakuta hayo hayo”alisema Kamanda Sabas
Pia aliongeza kuwa baada ya polisi kufika katika eneo la tukio walikuwa mwili huo ukiwa na suruali aina ya jeans ambayo ilikuwa imeshushwa hadi chini ya magoti na viungo vyake vikiwa vimenyofolewa
Hataivyo
jeshi hilolinaendela na upelelezi juu ya tukio hilona upelelzi wa
kumfahamu chanzo cha umati huo huku mwili wa marehemu ukiwa umehifadhiwa
katika chumba cha kuhifadhia maiti cha hospitali ya Mount Meru
Waziri akizungumza na Kamati ya Bunge
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira Dk Terezya Huvisa
akizungumza na Kamati ya Bunge ya Ardhi Maliasili na Mazingira kwenye
ukumbi wa Hazina kulia Mwenyekiti wa Kamati hiuo James Lembeli kushoto
Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Charles Kitwanga,Naibu katibu Mkuu
Eng Ngosi Mwihava,Mh Zakhia Megji kikao hicho kimefanyika leo Mjini
Dar es Salaam[Picha na Ali Meja
Baraza la Sanaa (BASATA) lawapa somo waandaaji wa Epic Bongo Star Search 2012
Na Mwandishi Wetu
BARAZA la Sanaa la Taifa (BASATA) limeendesha semina
ya siku moja kwa majaji wa shindano la Epic Bongo Star Search 2012 kwa kuwataka
kuzingatia maadili ya kazi zao.
Akitoa somo kwa majaji hao mratibu wa matukio wa
Basata Malimi Mashili aliwataka majaji hao kutambua kuwa asilimia kubwa
ya washiriki wanategemea zaidi msaada wao katika kukuza
vipaji.
Mashili aliwataka majaji hao kutambua kuwa mazingira
waliyotoka washiriki na kuangalia namna ya kuwasaidia kulingana na mikoa yao kwa
kuwa wapo ambao wana vipaji lakini wanatatizwa na suala la kuyazoea
mazingira.
Alisema kuwa kwa kuwa mwaka huu EBSS itaruhusu
washiriki wa miaka 16 hivyo ni vema zaidi wakazingatia suala la sauti kulingana
na umri wa mshiriki sababu watakuwepo wenye sauti za kitoto
pia.
Pia aliwataka majaji hao kuhakikisha kuwa hawatoi aina
yoyote ya upendeleo na wala kuwa karibu zaidi na baadhi ya washiriki wa shindano
hilo.
Pia alisisitiza kuwa majaji wanalo jukumu kubwa la
kuwaelekeza namna ya kuimba, kuvaa, kujiheshimu na usafi wa mwili
pia.
“Hiii ni semina ya kuwekana sawa tu kwa kuwa hili
shindano lipo kwa muda mrefu na majaji mmekuwa mkifanya vema, kwa niaba ya
BASATA napenda kuchukua muda huu kuwataka muwe makini katika kuzingatia maadili
haya niliyoyasema na hata mengine pia”alisema Mashili.Naye Mkurugenzi wa
Berchmark Production inayoandaa shindano hilo Ritha Paulsen alisema kuwa semina
hiyo ni muhimu kwa majaji kwa kuwa muda mzuri wa kukumbushana
mambo muhimu yahusuyo muziki.
Epiq Bongo Star Search mwaka huu inaanzia mkoani
Dodoma Juni 16 katika ukumbi wa Royal Village.
Majaji wa shindano hilo waliohudhuria ni pamoja na
Jaji Mkuu Ritha Paulsen, Master Jay, Salama pamoja na mratibu wa
EBSS kutoka Basata Vicky Temu.
habari zaidi ingia
www.elimuboratanzania. blogspot.com
MWENYEKITI WA KLABU YA SIMBA ASEMA: MKATABA WA YONDAN YANGA NI BATILI
Simba Sports club imesikitishwa na kitendo cha Young Africans
kuvunja taratibu za usajili kwa kumrubuni mchezaji wake Kelvin Patric
Yondani kwa kuzungumza naye na baadae kwa ushahidi wa picha kuonekana
wakimuandikisha makaratasi ambayo baadae imeripotiwa na vyombo vya
Habari kwamba alikuwa akisaini mkataba wa kuichezea timu hiyo ya Young
Africans.
Kwamba katika picha hiyo ameonekana mjumbe wa Young aliyejiuzuru
bwana Seif Ahmed na hilo lilitoa shaka kama utaratibu huo umefanywa na
klabu ya Young, lakini shaka hiyo imeondolewa pale ambapo tovuti ya
Young imetangaza kumsajili mchezaji huyo wa Simba SC, lakini zaidi ya
hilo picha inaonyesha fedha zikiwa zimewekwa mbele ya mchezaji jambo
linaloonyesha mazingira ya kurubuniwa kwani kwa utaratibu wa kifedha,
pesa nyingi kiasi hicho malipo yake yanashauriwa/yanapashwa kupitia
benki.
Mbali ya hayo picha hiyo inamuonyesha Kelvin akiwa katika jezi ya
mazoezi ya timu ya Taifa na yenye logo ya Kilimanjaro na kumbukumbu
zinaonyesha mkataba kati ya TBL na TFF tarehe 9/5/2012, kwa haraka
haraka tukio hilo limefanyika katika kipindi chini ya mwezi mmoja ingawa
taarifa za ushahidi zinaonyesha tukio hilo limetokea jana tarehe
6/6/2012.
Simba Sports Club ilipenda kuamini kwamba tukio hilo haliihusu
klabu ya Young kwani bwana Seif Ahmed alishajiuzuru kutoka kwenye kamati
ya Young Africans, kwani Young ni klabu kongwe na inayojua taratibu
zote za usajili.
Kwamba Simba Sports Club imeshawasiliana na jopo lake la mawakili
na inajiandaa kuishtaki klabu ya Young katika chombo husika cha mpira na
kudai adhabu ya kutopitisha majina yote ya usajili ya Young kwa mwaka
2012/2013 na miaka mingine miwili ijayo na Simba SC ipo tiyari
kufuatilia suala hili hadi katika mahakama ya mpira ya FIFA.
Kelvin Yondani ni mchezaji halali wa Simba Sc aliye na mkataba
hadi 31 mei 2014 mkataba ulioongezwa tarehe 23/12/2011 kuundeleza
mkataba wa awali uliokuwa unaisha tarehe 31/5/2012. Sheria za FIFA za
hadhi na uhamisho wa wachezaji ziko wazi katika kipengele cha 5 kifungu
kidogo cha 2 kinasema kwamba mchezaji atasajiliwa kuichezea timu moja
tu kwa wakati mmoja.
Imetolewa tarehe 7/6/2012.
MH. ISMAIL ADEN RAGE (MB)
MWENYEKITI
SIMBA SPORTS CLUB
Rais Dk. Shein akutana na Balozi wa Msumbiji na Sweden
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi,Dk.Ali
Mohamed Shein,akisalimiana na Balozi wa Msumbiji Nchini Tanzania Amour
Zakaria aliyefika Ikulu Mjini Zanzibar kumuaga Rais,kwa kumaliza muda
wake wa kazi nchini.[Picha na Ramadhan Othman,Ikulu.]
Mohamed Shein,akisalimiana na Balozi wa Msumbiji Nchini Tanzania Amour
Zakaria aliyefika Ikulu Mjini Zanzibar kumuaga Rais,kwa kumaliza muda
wake wa kazi nchini.[Picha na Ramadhan Othman,Ikulu.]
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi,Dk.Ali
Mohamed Shein,akizungumza na Balozi wa Msumbiji Nchini Tanzania Amour
Zakaria aliyefika Ikulu Mjini Zanzibar kumuaga Rais,kwa kumaliza muda
wake wa kazi nchini.[Picha na Ramadhan Othman,Ikulu.]
Mohamed Shein,akizungumza na Balozi wa Msumbiji Nchini Tanzania Amour
Zakaria aliyefika Ikulu Mjini Zanzibar kumuaga Rais,kwa kumaliza muda
wake wa kazi nchini.[Picha na Ramadhan Othman,Ikulu.]
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la
Mapinduzi,Dk.Ali Mohamed Shein,akisalimiana na Balozi wa Sweden Nchini
Tanzania Lennarth Hjelmaker,aliyefika Ikulu Mjini Zanzibar
kujitambulisha kwa Rais.[Picha na Ramadhan Othman,Ikulu.]
Mapinduzi,Dk.Ali Mohamed Shein,akisalimiana na Balozi wa Sweden Nchini
Tanzania Lennarth Hjelmaker,aliyefika Ikulu Mjini Zanzibar
kujitambulisha kwa Rais.[Picha na Ramadhan Othman,Ikulu.]
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la
Mapinduzi,Dk.Ali Mohamed Shein,akizungumza na Balozi wa Sweden Nchini
Tanzania Lennarth Hjelmaker,aliyefika Ikulu Mjini Zanzibar
kujitambulisha kwa Rais.[Picha na Ramadhan Othman,Ikulu.]
Mapinduzi,Dk.Ali Mohamed Shein,akizungumza na Balozi wa Sweden Nchini
Tanzania Lennarth Hjelmaker,aliyefika Ikulu Mjini Zanzibar
kujitambulisha kwa Rais.[Picha na Ramadhan Othman,Ikulu.]
GAMBIA KUWASILI LEO USIKU TAYARI KWA MPAMBANO WAO NA TAIFA STARS
Timu ya Taifa ya Gambia (The Scorpions) ambayo awali ilikuwa
iwasili nchini leo (Juni 7 mwaka huu) saa 1.40 asubuhi sasa itawasili
leo saa 9.20 usiku kwa ndege ya Kenya Airways tayari kwa ajili ya mechi
dhidi ya Taifa Stars.
The Scorpions ilipaswa kubadili ndege Dakar, Senegal jana usiku
lakini kukawa na ucheleweshaji (delay), hivyo ikashindwa kuwahi
Nairobi, Kenya ambapo ingeunganisha kwa ndege ya alfajiri kuja Dar es
Salaam.
Kikosi cha timu hiyo chenye wachezaji 22 wakiwemo tisa wanaocheza
mpira wa kulipwa nje ya nchi hiyo kitafikia kwenye hoteli Sapphire
iliyopo Mtaa wa Lindi na Sikukuu eneo la Kariakoo.
Wachezaji walioko katika msafara huo ni Musa Camara, Abdou
Jammeh, Momodou Futty Danso, Lamin Basmen Samateh, Ousman Koli, Pa
Saikou Kujabi, Mustapha Kebba Jarju, Yankuba Mal Ceesay na Demba
Savage.
Wengine ni Saihou Gassama, Alieu Darboe, Momodou Ceesay, Pa Modou
Jagne, Tijan Jaiteh, Bubacarr Sanyang, Christopher Allen, Musa Yaffa,
Sulayman Marr, Mamut Saine, Hamsa Barry, Ali Sowe, Omar Colley na
Saloum Faal.
PROGRAMU YA MAZOEZI YA GAMBIA
IJUMAA JUNI 8
01.00 asubuhi Mazoezi- Uwanja wa Karume
10.00 jioni Mazoezi- Uwanja wa Taifa
JUMAMOSI JUNI 9
04.00 asubuhi Mkutano na Waandishi wa Habari- Ukumbi wa TFF
10.00 jioni Mazoezi- Uwanja wa Taifa
Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Maalim Seif Sharif Hamad na Mwenyekiti Wa CUF Profesa ibrahim Lipumba Wahudhuria Mazishi Ya Mwenyekiti Mstaafu Wa CUF Marehemu Musobi Mageni
Makamu
wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Maalim Seif Sharif Hamad akitoa salaam
za pole kwa viongozi na chama cha Wananchi CUF na wananchi wa mkoa wa
Mwanza katika mazishi ya Mwenyekiti mstaafu wa chama hicho, marehemu
Musobi Mageni
Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar na katibu mkuu wa CUF, Maalim Seif Sharif Hamad akiweka udongo kwenye kaburi la
Mwenyekiti mstaafu wa chama hicho, marehemu Musobi Mageni ,kulia kwake
ni Mwenyekiti wa Cuf Profesa ibrahim Lipumba ambao wote walijumuika
na viongozi na chama cha Wananchi CUF na wananchi wa mkoa wa Mwanza
katika mazishi ya Mwenyekiti mstaafu wa chama hicho, marehemu Musobi
Mageni
--
Makamu
wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Maalim Seif Sharif Hamad amejumuika na
viongozi wa chama cha Wananchi CUF na wananchi wa mkoa wa Mwanza katika
mazishi ya Mwenyekiti mstaafu wa chama hicho, marehemu Musobi Mageni
huko kijijini kwao Ngudu, Wilaya ya Kwimba mkoani Mwanza.
Katika mazishi hayo, pia alihudhuria Mwenyekiti wa chama hicho,
Profesa Ibrahim Lipumba, Makamu Mwenyekiti, Machano Khamis Ali, pamoja
na wajumbe wa Baraza Kuu la Uongozi Taifa, wakiwemo Waziri wa Afya
Zanzibar, Juma Duni Haji na Mkurugenzi wa Mawasiliano na Haki za
Binaadamu, Salum Bimani.
Marehemu Musobi alifariki Dunia Mei 30, mwaka huu nyumbani kwake
Ngudu baada ya kusumbuliwa na maradhi ya shinikizo na damu na sukari
kwa muda mrefu.
Marehemu alihamia chama cha Wananchi CUF mwaka 1994 na
kuchaguliwa kuwa Mwenyekiti Taifa mwaka 1995 hadi 1999 alipostaafu na
kubaki kuwa Mjumbe wa kudumu wa Baraza Kuu la Taifa na Mkutano Mkuu wa
chama hicho hadi kifo chake.
Katika uhai wake, marehemu aliwahi kuwa Waziri wa Ardhi, Nyumba
na Maendeleo Mijini kuanzia mwaka 1972 hadi 1975, mwaka 1976 hadi 1978
Mkurugenzi wa Utumishi na Utawala Rajan Industries Ltd. Nafasi nyengine
ni alizowahi kushikilia ni Ubunge na Mkuu wa Wilaya katika wilaya ya
Chunya, Kahama na Muleba.
Akitoa salamu za rambirambi, Makamu wa Kwanza wa Rais, ambaye pia
ni Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi CUF, Maalim Seif Sharif Hamad
wakati wa mazishi alisema, marehemu alikuwa kisima cha busara na mwenye
hekima kubwa na ndio maana viongozi wa CUF walikuwa wakikimbilia kwake
kuchota ushauri wake.
“Huu ni msiba mkubwa sio tu kwa familia yake, bali kwa chama chetu na kwa serikali zote mbili”, alisema Maalim Seif.
Marehemu ambaye alizaliwa mwaka 1930, ameacha wajane wawili, watoto 15, wajukuu 28 na vitukuu sita.
Na
Khamis Haji
Ofisi Ya Makamu wa Kwanza Wa Rais Zanzibar
MILIONI 421.8 ZAPATIKANA KUCHANGIA MPANGO WA ELIMU KATA YA KIPAWA JIJINI DAR ES SALAAM
Mbunge wa Jimbo la Segerea, Dk. Makongoro Mahanga (kulia), Meya wa
Manispaa ya Ilala, Jerry Silaa (kushoto) na Mwenyeji wa harambee ya
kuchangia mpango wa elimu wa Kata ya Kipawa, Diwani wa Kata hiyo Bonah
Kaluwa, wakimuongoza Waziri Mkuu wa zamani Edward Lowassa ambaye
alikuwa mgeni rasmi kuingia ukumbini Katika hafla iliyofanyika jana
usiku ndani ya hoteli ya Kilimanjaro (Kempiski hotel) jijini Dar es
Salaam .
(PICHA NA PHILEMON SOLOMON WA FULLSHANGWE)
(PICHA NA PHILEMON SOLOMON WA FULLSHANGWE)
Wadau mbalimbali wakiwa kwenye harambee hiyo
Diwani wa Kata ya Kipawa Bonah Kaluwa, akitoa neno la shukurani kabla ya kuanza kwa harambee hiyo.
Mgeni rasmi wa Hharambee hiyo akimpa mkono wa asante mwakilishi wa
kampuni ya Home Shopping Centre Bi Madiha Al Harthy (kushoto),Salma
baada ya kuchangia sh. milioni 22.
Mkurugenzi wa SONGAS Limited Bw;Christopher Ford(katikati),akimkabidhi
mfano wa hundi yenye thamani ya dolla za kimarekani 10,000, mgeni rasmi
wa harambee hiyo.kushoto meneja
rasilimali Songas Bi Agatha Keenja.
Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Mkoa wa Shinyanga, Hamisi Mgeja
(katikati) akipongezwa na Mgeni rasmi wa harambe hiyo baada ya
kuchangia sh. 500,000.
eya wa Manispaa ya Ilala, Jerry Silaa (kushoto), akimkabidhi mfano wa
hundi yenye thamani ya sh.milioni 10, Waziri Mkuu wa zamani, Edward
Lowassa, aliyekuwa mgeni rasmi katika harambee ya kuchangia mpango wa
elimu Kata ya Kipawa, iliyofanyika Dar es Salaam juzi. Fedha hizo
zilitolewa na Manispaa hiyo ambapo zaidi ya sh. milioni 400
zilipatikana.
Na Dotto Mwaibale
WAZIRI Mkuu wa zamani , Edward Lowassa, ameendeleza kuwa mstari wa mbele
katika harakati zake za kuchangisha mamilioni ya fedha baada ya
kuchangisha Sh.421,850,000 kwa ajili ya kuboresha Mfuko wa Elimu Kata ya
Kipawa katika Manispaa ya Ilala Jijini Dar es Salaam.
Lowassa ambaye ni mbunge wa Monduli (CCM), aliendesha harambee hiyo juzi
katika hafla iliyofanyika Hoteli ya Kempiski Jijini Dar es Salaam
ambapo yeye mwenyewe alichangia Sh.milioni 10.
Katika harambee hiyo miongoni mwa makampuni yaliyochangia kiasi kikubwa
ni Lion Club Sh.milioni 70, Home Shipping Center Sh.milioni 22, African
Barrick Gold Dola 10,000, Songas Dola 10,000, Maersk Sea Line
ilichangia Sh.Miliono 90, na Mbunge wa Sengerema, William Ngeleja
alichangia milioni Sh.10.
Wengine waliochangia ni madiwani, viongozi wa Chama Cha Mapinduzi,
Chadema, taasisi za watu binafsi na mtu mmoja mmoja ambapo Radio Clauds
walitoa muda wa hewani wa kutangaza mpango huo wenye thamani ya sh.
milioni 12.
Akizungumza kabla ya kuendesha harambee ya kuchangisha, aliwataka Wakuu
wa Wilaya na Wakurugenzi wa Halmashauri kuendelea kuwahamasisha
wananchi kuwekeza katika kuchangia sekta ya elimu.
Lowassa alimpongea Diwani wa Kata ya Kipawa, Bonnah Kaluwa, kwa jitihada
zake alizozionyesha za kuchangia elimu na kuwataka madiwani wengine
kuiga mfano huo.
Diwani wa Kata ya Kipawa, Bonnah Kaluwa, kwaupande wake alisema shule
saba za Msingi na Sekondari zilizopo kata hiyo zinakabiliwa na matatizo
lukuki ikiwemo upungufu wa vyumba vya madarasa hali inayosababisha
wanafunzi kati ya 140 hadi 160 kusomea katika darasa moja.
“Shule za kata yangu kwa kweli zinakabiliwa na changamoto nyingi, kwa
mfano Shule ya Msingi ya Majani ya Chai ina vyumba vya madarasa nane
wakati wanafunzi waliopo ni 2,200, Shule ya Msingi ya Minazi Mirefu
madarasa yake yaliyopo ni machakavu pia hayatoshelezi,”alisema Kaluwa.
Kaluwa alisema jitihada nyingine zilizofanywa katika kutafuta pesa kwa
ajili ya kuziboresha shule hizo ambapo Machi 17 mwaka huu kuliitishwa
matembezi ya hisani yaliyoongozwa na mke wa Rais Mama Salma Kikwete.
Aliongeza kuwa katika hafla hiyo kiasi cha shilingi milioni 15
kilichangwa na wadau mbalimbali ambapo kati ya hizo Sh.Milioni 3
zilitolewa na Mke wa Rais Mama Salma Kikwete na Clouds Media Group
ambao walitoa shilingi milioni moja na wanafunzi kadhaa wa shule za
msingi na sekondari.
Mbunge wa Jimbo la Segerea Dk.Makongoro Mahanga aliwashukuru wadau
waliojitokeza kuchangia kata hiyo ambayo ipo katika jimbo lake na
kuwataka wadau wengeni kuchangia kata zingine ili kukabiliana na
matatizo hayo katika shule mbalimbali
Tawi la CHADEMA Washington DC Nchini Marekani Lazidi Kuvuna Wanachama Wapya
Linda Bezuidenhout (LB) furaha baada ya kuvua kamba kuvaa kwanda na kuchukua kadi kuwa mwanachama kamili wa Chama Cha Demokrasia Chadema.
Mwenyeketi wa tawi la Tawi la Chama Cha Demokrasia CHADEMA
Washington DC Mhe. Kalley Pandukizi, pamoja na katibu wake Mhe. Libe
Mwang'ombe akimkabidhi rasmi mwanacham mkareketwa ambae ni mwana
mitindo Linda Bezuidenhout (LB) kati ya uwanachama wa chama cha
Demokrasia Chadema katika ofisi ya tawi la Tawi la Chama Washington
DC.
Mwenyeketi wa Tawi la Chama Cha Demokrasia CHADEMA Washington
DC Kalley Pandukizi akiwa na katibu wachama hicho,Ndugu Libe Mwang'ombe
alipotoa kadi rasmi kwa Beautician maharufu na designer wa kitanzan
Linda Bezuidenhout (LB)
Viongozi wa tawi la chadema Washington DC wakipata Champagne
Mwenyeketi wa tawi la Tawi la Chama Cha Demokrasia CHADEMA
Washington DC Mhe. Kalley pamoja na katibu wake Mhe. Libe Mwang'ombe
wakipata picha ya pamoja na Linda Bezuidenhout Atlanta, Georgia na
wanachama wa tawi la chadema Washington DC.
Katika
miaka ya nyuma Linda aliwahi kusponsor matukio mbali mbali kwenye
miaka ya 1990 wengi wao wakimjua kwa Linda Express Nchini Tanzania
ambae ambaye hivisasa anajishughulisha na biashara ya nguo za kiume milanovita.com pamoja na zakike ambazo anadesign mwenyewe kwa brand name ya Linda kutoka Atlanta, Georgia Nchini Marekani.Picha na Mdau Wa Swahilivilla
TANGAZO LA OFISI YA MKUU WA MKOA WA RUKWA :UPOTEVU WA VITABU ISHIRINI (20) VYA LESENI YA BIASHARA
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Rukwa inapenda kuutangazia Umma kuwa imepotelewa na vitabu ishirini (20) vya leseni za biashara vilivyopotea tarehe 22 Mei 2012 katika moja ya Daladala Jijini Dar es Salaam.
Vitabu hivyo vilivyotolewa na Wizara ya Viwanda na Biashara vikiwa na kumbukumbu namba 1389501 mpaka 1391500.
Kwa yeyote atakayeona vitabu hivyo au kuvinunua anaombwa avipeleke kituo chochote cha polisi kilicho karibu yake au kutoa taarifa juu ya mwenye navyo katika kituo hicho.
Ifahamike kuwa vitabu hivyo ni batili hivyo haviruhusiwi kutumika kwa namna yeyote ile. Na atakayethibitika kuvitumia atachukuliwa hatua kwa mujibu wa sheria zilizowekwa.
Ewe mfanyabiashara, epuka manunuzi na matumizi ya vitabu vyenye namba tajwa hapo juu kwa usalama wa biashara yako.
Kwa mawasiliano tunaomba mtumie namba zetu hapo juu.
Tunaomba ushirikiano wenu.
IMETOLEWA NA
HAMZA TEMBA
AFISA HABARI MKOA WA RUKWA
07/06/2012
YONDAN AKIMWAGA WINO YANGA NA KITITA CHAKE CHA MIL.30
KELVIN
Patrick Yondan, beki wa kati wa Simba amekana kusaini mkataba wowote na
Simba na amesema yeye amesaini Yanga tu mkataba wa miaka miwili.
Yondan amesema Simba wanampakazia kusaini mkataba mpya na anataka wapenzi wote wa soka Tanzania watambue kwamba kuanzia sasa yeye ni mchezaji halali wa Yanga.
Yondan aliikana Yanga awali kwa sababu walimsainisha fomu bila kumpa fedha, lakini leo amepewa Milioni 30 zake taslimu na amemaliza kila kitu.
Yondan amesema Simba wanampakazia kusaini mkataba mpya na anataka wapenzi wote wa soka Tanzania watambue kwamba kuanzia sasa yeye ni mchezaji halali wa Yanga.
Yondan aliikana Yanga awali kwa sababu walimsainisha fomu bila kumpa fedha, lakini leo amepewa Milioni 30 zake taslimu na amemaliza kila kitu.
Kwa hisani ya www.mamapipiro.blogspot.com
TIKA itaboresha huduma Ilala- Meya wa Ilala Jerry Slaa
Meya wa Manispaa ya Ilala Mh. Jerry Slaa akufungua
semina ya Mpango wa bima ya Afya unaojulikana kama TIKA uliobuniwa na
Mfuko wa Bima wa Afya (NHIF) inayotolewa kwa madiwani wa Manispaa hiyo
inayofanyika kwenye ukumbi wa Arnautoglo Mnazi Mmoja jijini Dar es
salaam asubuhi hii, kushoto ni Naibu Mkurugenzi wa NHIF Bw Khamis Mdee
na kulia ni Kaimu Mkurugenzi wa Manispaa ya Ilala Ellias Mwasabwite.
Naibu Mkurugenzi wa NHIF Bw Khamis Mdeeakizungumza katika semina hiyo
kulia ni Kaimu Mkurugenzi wa Manispaa ya Ilala Ellioth Mwasabwite na
katikati ni Meya wa Ilala Mh. Jerry Slaa.
Wakurugenzi na maafisa kutoka Mfuko wa Bima wa Afya wakiwa katika semina hiyo leo.
Madwani wanaoshiriki katika semina hiyo wakifuatilia kwa makini mada katika semina hiyo.
Meya wa Manispaa ya Ilala Mh. Jerry Slaa kushoto ni Naibu Mkurugenzi wa
NHIF Bw. Khamis Mdee na kulia ni Kaimu Mkurugenzi wa Manispaa ya Ilala
Ellias Mwasabwite.
Meya wa Manispaa ya Ilala Mh. Jerry Slaa kushoto ni Naibu Mkurugenzi wa
NHIF Bw. Khamis Mdee na kulia ni Kaimu Mkurugenzi wa Manispaa ya Ilala
Ellias Mwasabwite.
No comments:
Post a Comment